Chakula

Vyakula vyenye asili ya mimea.
Aina za nyama.

Chakula (kifupi cha "kitu cha kula", kutoka kitenzi "kula") ni kile kinacholiwa na watu kwa kudumisha na kustawisha uhai wao. Ni kwamba mwili unahitaji virutubishi, nishati na maji. Hayo yote hupatikana katika chakula.

Virutubishi vya mwili ni hasa yafuatayo:

Protini, mafuta na wanga huleta nishati ya mwili. Vilevile hukuza mwili yaani katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula (tumboni) vinapasuliwa kwa sehemu asilia zake na kuingizwa katika muundo wa seli za mwili.

Chakula kinaweza kutoka kwenye mimea au kwenye wanyama. Sehemu ya mahitaji yanatoka pia moja kwa moja kwenye mazingira bila kupitia mimea wala wanyama, hasa madini, kwa mfano chumvi.

Lakini chakula si kazi ya kibiolojia na kifiziolojia pekee, bali kina upande wa kiutamaduni na kijamii vilevile.

Kila nchi ina chakula chake na watu wamezoea vyakula pamoja na namna ya kutayarisha vyakula vyao.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search