Historia ya Afrika

Mataifa ya Afrika kabla ya ukoloni kutoka nyakati tofauti
Mataifa ya Afrika kabla ya ukoloni.

Historia ya Afrika ni historia[1] ya bara hilo lililo asili ya binadamu wote.

Ramani ya sasa ya kisiasa ya Afrika (ikijumuisha kusini mwa Sahara na Afrika kaskazini).
Ramani ya kisiasa ya Afrika nzima leo.

Kwa ujumla, historia ni kumbukumbu ya maisha ya mwanadamu duniani, hasa ile tarehe iliyosajiliwa na kuhifadhiwa katika vitabu, maandishi mbalimbali, na simulizi au hekaya za mapokeo. Ingawa historia iliyobebwa katika simulizi na hekaya huchukuliwa na baadhi kuwa haina nguvu kwa kukosa ithbati ya maandishi, bado hivi ni vyanzo muhimu vya historia. Mara nyingi historia iliyoko katika maandishi huwa imehifadhiwa katika simulizi na hekaya kwa muda mrefu kabla ya kuandikwa.

  1. Wakati mwingine neno "tarehe" latumiwa badala ya historia, kutokana na maana asilia ya neno la Kiarabu "tarih"

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search