Jamhuri ya Watu wa China


Zhōnghuá Rénmín Gònghéguó

Jamhuri ya Watu wa China
Bendera ya China Nembo ya China
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa:
Wimbo wa taifa: Maandamano ya wale wanaojitolea - ''Yìyǒngjūn Jìnxíngqǔ''
Lokeshen ya China
Mji mkuu Beijing
9,596,961) 39°55′ N 116°23′ E
Mji mkubwa nchini Shanghai
Lugha rasmi Kimandarini1 (Putonghua)
Serikali Ujamaa jamhuri ya chama kimoja2
Xi Jinping
Li Keqiang
Tarehe za kihistoria
Utawala wa nasaba ya Shang
Utawala wa nasaba ya Qin
Jamhuri ya China
Jamhuri ya Watu wa China ilitangazwa

1766 KK
221 KK
10 Oktoba 1911
1 Oktoba 1949
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
km² 9,596,961 km² (ya 33)
0.282
Idadi ya watu
 - Januari 2020 kadirio
 - 2010 sensa
 - Msongamano wa watu
 
1,400,000,0004 (ya 1)
1,339,724,852
145/km² (ya 83 (2))
Fedha Renminbi Yuan5, 2 (CNY)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+8)
not observed (UTC+8)
Intaneti TLD .cn2
Kodi ya simu +862

-

1 Pamoja na Kimandarini kile cha Kikantoni ni lugha rasmi katika Hong Kong na Macau. Kiingereza ni pia lugha rasmi katika Hong Kong na Kireno huko Macau. Vilevile kuna lugha za kieneo yanayotumiwa rasmi kama vile Kiuyghur huko Xinjiang, Kimongolia katika jimbo la Mongolia ya Ndani, Kitibet huko Tibet na Kikorea katika mkoa wa Yanbian.


China (pia: Uchina, Sina; kirefu: Jamhuri ya Watu wa China) ni nchi kubwa ya Asia ya Mashariki ambayo ndiyo nchi yenye watu wengi kuliko zote duniani.

China imepakana na Vietnam, Laos, Myanmar, India, Bhutan, Nepal, Pakistan, Afghanistan, Tajikistan, Kyrgyzstan, Kazakhstan, Urusi, Mongolia, Korea ya Kaskazini.

Kuna pwani ndefu kwenye Bahari ya Kusini ya China na Bahari ya Mashariki ya China ambazo ni bahari ya kando ya Pasifiki.

China kuna makabila 56 tofauti. Wahan ndio kabila kubwa zaidi nchini China kwa idadi ya watu ikiwa na asilimia 92.

Lugha rasmi ni Kichina cha Mandarin kinachotumiwa na asilimia 70 za wananchi.

Siasa inatawaliwa na chama cha kikomunisti.

Mji mkuu ni Beijing lakini Shanghai ndio mji mkubwa zaidi.

Hong Kong iliyokuwa koloni la Uingereza na Macau iliyokuwa koloni la Ureno ni maeneo ya China yenye utawala wa pekee.

Taiwan na visiwa vingine vya Jamhuri ya China vinatazamwa na serikali ya Beijing kuwa majimbo yake lakini vimekuwa kama nchi ya pekee tangu mwaka 1949.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search