John Magufuli

John Pombe Magufuli
John Pombe Joseph Magufuli
John Pombe Joseph Magufuli
Rais wa Tanzania
Tarehe ya kuzaliwa 29 Oktoba 1959
Tarehe ya kifo 17 Machi 2021
Chama CCM
Dini Ukristo (Kanisa Katoliki)
Elimu yake Mwanakemia
Digrii anazoshika Shahada ya Uzamivu
Kazi Mwanasiasa


John Pombe Joseph Magufuli (29 Oktoba 1959 - 17 Machi 2021) alikuwa rais wa tano wa Tanzania, akitokea katika chama cha Mapinduzi CCM. Aliongoza kwa muda wa miaka mitano na nusu hadi kifo chake[1].

Aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo la Biharamulo Mashariki katika bunge la kitaifa huko nchini Tanzania na tangu mwaka 2010 aliteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi.[2]

Tarehe 12 Julai 2015 alichaguliwa kuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi akiwa na mgombea mwenza Samia Suluhu Hassan.

Tarehe 29 Oktoba 2015 Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilimtangaza kuwa rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushindi wa kura 8,882,935 sawa na 58.46% pamoja na makamu wa rais Samia Suluhu Hassani.

Tarehe 5 Novemba 2015 aliapishwa kama rais wa tano wa Tanzania, ingawa upinzani haukukubali matokeo hayo.

Baada ya uchaguzi wa tarehe 28 Oktoba 2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilimtangaza tena mshindi pamoja na makamu wa rais Samia Suluhu Hassan kwa kura 12,516,252 sawa na 84.4% ingawa kulikuwa na malalamiko makubwa[3].

  1. https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mabeyo-asimulia-kabla-baada-kifo-cha-magufuli-4558824
  2. "Mengi kuhusu John Pombe Joseph Magufuli". 18 Februari 2008. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-10-20. Iliwekwa mnamo 11 Novemba 2011.
  3. "Magufuli wins re-election in Tanzania; opposition cries foul", Al Jazeera, 30 October 2020 https://www.aljazeera.com/news/2020/10/30/magufuli-wins-re-election-in-tanzania-says-electoral-commission

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search