Juma

Juma (kutoka neno la Kiarabu) au wiki (kutoka Kiingereza "week") ni kipindi cha siku saba. Kila siku ina jina lake.

Katika mwaka wa kalenda ya Gregori mna majuma 52 pamoja na siku moja au mbili za ziada. Hesabu ya majuma inaendelea mfululizo bila ya kuanza upya wakati wa mwaka mpya.

Ufuatano wa majuma haulingani na mgawanyo mwingine wa wakati kwa njia ya miezi au mwaka.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search