Kanisa kuu

Upande wa mbele wa Basilika kuu la Mt. Yohane huko Laterano wakati wa usiku. Ndilo kanisa kuu la Roma. Juu ya paa, pamoja na nyingine, kuna sanamu ya Yesu Mkombozi tena 12 za Mitume wa Yesu.
Kanisa kuu la Kilutheri la Helsinki, Ufini.
Kanisa kuu la Kikatoliki huko Salta, Argentina.

Kanisa kuu ni jina la heshima la jengo la ibada la madhehebu mbalimbali ya Ukristo ambalo Askofu wa jimbo (dayosisi) fulani analitumia kwa kawaida kutekeleza kazi yake kama mchungaji mkuu wa waamini wake, kama vile kuhubiri na kufundisha Neno la Mungu, kutakasa watu kwa sakramenti na sala mbalimbali na kuwaunganisha wote katika kumfuata Yesu pamoja.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search