Karolo Mkuu

Sarafu ya mwaka 814 inayomwonyesha Karolo Mkuu
(Maandishi yanasema: "KAROLUS IMPAUG" yaani Karolus Imperator Augustus.
Karolo Mkuu na Papa Adrian I.

Karolo Mkuu (kwa Kilatini: Carolus Magnus; kwa Kijerumani: Karl der Große; kwa Kifaransa: Charlemagne) alizaliwa tarehe 2 Aprili mwaka 742 na kufariki tarehe 28 Januari 814; alikuwa kwanza mfalme wa Wafranki halafu Kaizari wa Dola takatifu la Roma aliloanzisha.

Pengine anaitwa "baba wa Ulaya" kwa kuwa milki yake iliunganisha nchi zilizoanzisha Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya (chanzo cha Umoja wa Ulaya) katika karne ya 20.

Tangu kale anaheshimiwa na baadhi ya Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 28 Januari.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search