Katerina wa Aleksandria (kwa Kigiriki ἡ Ἁγία Αἰκατερίνα ἡ Μεγαλομάρτυς; 282-305 hivi) alikuwa bikira Mkristo wa Aleksandria, Misri ambaye aliuawa kwa amri ya kaisari Maxentius mwanzoni mwa karne ya 4[1].
Kadiri ya mapokeo, alikuwa wa ukoo maarufu[2] tena msomi. Kisha kuongokea Ukristo akiwa na umri wa miaka 14, aliongoza watu mia kadhaa kumfuata katika dini hiyo[3].
Tangu alipofia dini anaheshimiwa na Wakristo wa madhehebu mbalimbali kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 24 Novemba au 25 Novemba.[4][5][6]
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search