Kicheki

Kicheki ni lugha ya Kislavoni katika familia ya lugha za Kislavoni cha Magharibi inayotumiwa nchini Ucheki. Pia kuna wasemaji takriban milioni mbili nje ya Ucheki.

Kicheki ni lugha ya karibu na Kislovakia na Kisorbi. Kinaandikwa kwa alfabeti ya Kilatini.

Wageni hushtuka mara nyingi wakiona maneno bila vokali, kwa mfano sentensi "Strč prst skrz krk". Sababu yake ni kwamba herufi za r na l zinaweza kuhesabiwa kama silabi (utaratibu unaofanana na "m" kama mwanzo wa neno mbele ya konsonanti katika lugha za Kibantu: m-fano, M-swahili).

Sarufi inapanga nomino zote katika jinsia tatu.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search