Kilimo

Michoro ya Misri ya Kale.
Trekta.

Kilimo ni uzalishaji wa mazao kwenye mashamba.

Kilimo kina maana pana inayojumuisha mifumo ya uzalishaji mimea, ufugaji wa wanyama, na uvuvi wa samaki. Mara nyingi kilimo cha mimea kinaenda sambamba na ufugaji wa wanyama.

Watu hupanda mimea na kuitunza hadi mavuno hasa kwa uzalishaji wa chakula cha binadamu na lishe ya wanyama, lakini pia kwa shabaha ya kupata malighafi mbalimbali zinazotumiwa kwa kutengeneza nguo za watu.

Siku hizi kilimo kinalenga pia nishati ya mimea.

Mtu anayejihusisha na kilimo huitwa mkulima.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search