Kitale | |
Mahali pa mji wa Kitale katika Kenya |
|
Majiranukta: 1°01′0″N 35°0′0″E / 1.01667°N 35.00000°E | |
Nchi | Kenya |
---|---|
Kaunti | Trans-Nzoia |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 106,187 |
Kitale ni mji wa Kenya katika Bonde la Ufa la Afrika Mashariki. Ni makao makuu ya kaunti ya Trans-Nzoia.
Mji uko mita 1900 juu ya usawa wa bahari.
Hifadhi ya Taifa ya Saiwa Swamp iko karibu na mji, ambao unajulikana pia kwa makumbusho ya Kitale [1].
Mazao ya sokoni inayokuzwa katika sehemu hii ni majani ya chai, kahawa, pareto, alizeti, maharagwe na mahindi. Kitale ni soko la mazao ya kilimo na kituo cha kilimo cha mseto.
Mji huu ulianzishwa mwaka wa 1908 na Wazungu walowezi. Reli ya Uganda kutoka Eldoret ilifika Kitale mwaka wa 1926 na ilichangia kukuza mji huu. Kadiri ya sensa ya mwaka 2009, mji ulikuwa na wakazi 106,187[2].
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search