Lugha za Kiturki

Usambaji wa lugha za Kiturki katia Asia

Lugha za Kiturki ni kundi la lugha zaidi ya 30 zinazozungumzwa kutoka Ulaya ya Mashariki hadi Asia ya Kati na watu milioni 210. Zinahesabiwa kuwa sehemu za lugha za Kialtai pamoja na Kichina, Kimongolia, Kijapani na Kikorea. Wasemaji wa lugha za Kiturki husikizana kwa kiasi kikubwa. Lugha ya Kiturki inayojulikana zaidi kimataifa pia yenye wasemaji wengi ni Kituruki cha Uturuki.

Asili ya wasemaji wa lugha za Kiturki inadhaniwa kuwa sehemu za Mongolia. Kati ya karne za 6 hadi 10 walisambaa hadi Asia ya Magharibi na baada ya kutwaa Milki ya Bizanti waliingia pia katika Ulaya ya kusini-mashariki.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search