Makanisa Katoliki ya Mashariki

Askofu Mkatoliki wa Mashariki akiadhimisha Liturujia ya Kimungu huko Prešov (Slovakia).

Makanisa Katoliki ya Mashariki ni madhehebu 23 ya Ukristo ambayo yanafuata mapokeo mbalimbali ya Mashariki katika ushirika kamili na Askofu wa Roma (Papa), hivyo pia na Kanisa Katoliki lote duniani.

Mapokeo hayo ni hasa yale ya Aleksandria (Misri), Antiokia (kihistoria jiji la Siria, leo nchini Uturuki), Konstantinopoli (kihistoria jiji la Ugiriki, leo nchini Uturuki), Armenia na Wakaldayo (kihistoria Mesopotamia, leo Iraq).

Baadhi ya mapokeo hayo yamezaa matawi, kama ya Misri yale ya Ethiopia na Eritrea.

Pamoja na hayo, kama Makanisa ya Waorthodoksi, hayo pia yanaambatana na utamaduni wa taifa, na kuyafanya yagawanyike kiutawala hata kama teolojia, liturujia n.k. zinaendelea kuwa zilezile kadiri ya mapokeo.

Kwa jumla yanakubali kuwa mapadre watu waliooa lakini hawana maaskofu waliooa.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search