Meno

Meno bora
Meno ya hatari!

Meno ni viungo vya mwili vilivyopo kinywani vyenye kazi ya kutafuna yaani kumega chakula.

Meno hupatikana kwa vertebrata (wanyama wenye uti wa mgongo). Nje ya kutafuna chakula hutumiwa pia kama silaha za kujilinda au kushambulia wanyama wengine. Wanyama kadhaa huwa na meno nje ya mdomo kwa matumizi kama silaha (mfano: tembo) yanayoweza kutumiwa pia kama vifaa vya kuchimba (mfano: nguruwe-mwitu).

Kwa binadamu meno hupatika kinywani tu. Kazi kubwa ya meno kwa binadamu ni katika umeng'enyaji wa chakula anachokula na mara chache katika kusaidia kukata vitu mbalimbali kama kutatua kitambaa au kukata kamba au waya. Binadamu ana aina mbalimbali za meno zinazomsadia kula vyakula vya aina mbalimbali kama vile vya mimea na nyama. Kwa kawaida mtu mzima huwa na meno thelathini na mbili.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search