Moyo ni ogani ya mwili inayoendesha mzunguko wa damu mwilini. Kazi yake ni kama pampu ya damu. Hali halisi ni misuli inayosukuma damu kwenye mishipa kwa njia ya kujikaza.
Mioyo ya mamalia pamoja na binadamu huwa na pande mbili. Upande wa kulia unasukuma damu kwenda mapafu inapopokea oksijeni; upande wa kushoto unazungusha damu katika sehemu nyingine za mwili pale ambako oksijeni inahitajika.
Moyo ni ogani ya lazima kwa uhai.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search