Moyo

Moyo wa binadamu baada ya kutolewa kwenye maiti kwa utafiti wa kiganga.
Moyo kama ishara ya upendo.
Muundo wa moyo wa binadamu
*1 Vena kava ya juu (damu inaingia kutoka mwilini)
*2 ateri ya mapafu (damu inatoka kwenda mapafu)
*3 vena ya mapafu (damu inarudi kutoka mapafu)
*4 Vali mitralia - 5 Vali ya aorta
*6 Ventrikali kushoto - 7 Ventrikali kulia
*8 Atiria kushoto - 9 Atiria kulia
*10 Aorta (damu inatoka kwenda mwilini)
*11 Vali kwa mapafu - 12 Vali triskupidia
*13 Vena kava ya chini (damu inaingia kutoka mwilini)

Moyo ni ogani ya mwili inayoendesha mzunguko wa damu mwilini. Kazi yake ni kama pampu ya damu. Hali halisi ni misuli inayosukuma damu kwenye mishipa kwa njia ya kujikaza.

Mioyo ya mamalia pamoja na binadamu huwa na pande mbili. Upande wa kulia unasukuma damu kwenda mapafu inapopokea oksijeni; upande wa kushoto unazungusha damu katika sehemu nyingine za mwili pale ambako oksijeni inahitajika.

Moyo ni ogani ya lazima kwa uhai.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search