Mtaguso wa kwanza wa Laterano

Basilika la Mtakatifu Yohane huko Laterano ambamo mtaguso ulifanyika.

Mtaguso wa kwanza wa Laterano unahesabiwa na Kanisa Katoliki mtaguso mkuu wa tisa katika historia yake, wa kwanza kufanyika Magharibi. Ulianza tarehe 18 Machi ukamalizika tarehe 11 Aprili 1123.

Mahali pake ni kwenye Kanisa kuu la Roma huko Laterano, mtaa wa Roma (Italia) alipokuwa anaishi askofu wake. Hukohuko baadaye ilifanyika mitaguso mingine minne ya Karne za Kati. Umuhimu wa kanisa hilo ulipungua hasa baada ya Papa kuhamia Vatikano.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search