Mtaguso wa nne wa Konstantinopoli

Mtaguso wa nne wa Konstantinopoli ni jina linalotumiwa na Wakristo kwa namna tofauti, kadiri wanavyokubali au kukataa uhalali na uekumeni wa mitaguso fulanifulani.

Kanisa Katoliki linahesabu kuwa Mtaguso mkuu wa nne ule uliofanyika tangu tarehe 5 Oktoba 869 hadi 28 Februari 870.

Uliitishwa na Kaisari Basili I wa Bisanti na Papa Adrian II (867-872) kwa sababu mwisho wa ikonoklastia katika sinodi ya mwaka 843 ulikuwa umeacha athari kubwa katika Kanisa la Mashariki.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search