Mvua ya mawe

Matone ya mvua ya mawe.
Kipande kikubwa cha barafu (kipenyo chake ni sentimeta 6) kilichotokea kwa kuungana kwa matone madogo zaidi hewani

Mvua ya mawe (kwa Kiingereza hail) ni aina ya mvua ambayo matone ya maji yamefika kwenye uso wa ardhi kwa umbo la vipande vya barafu. Inatokea wakati matone ya maji ya mvua yanapita kwenye hewa baridi na kuganda hadi kuwa barafu.

Hali halisi mvua inayonyesha si mawe bali vipande vya barafu.

Tone zito zaidi lililowahi kupimwa lilinyesha sehemu za Gopalganj (Bangladesh) tarehe 14 Aprili 1986, likiwa la kilogramu 1.02[1]. Kericho nchini Kenya penye mvua ya radi mara nyingi[2] ni mahali ambako mvua ya mawe inanyesha zaidi kushinda sehemu nyingine za Dunia[3].

  1. World heaviest hailstone, tovuti ya Arizona State university. Anguko la mvua ya mawe ile liliua pia watu huko Bangla Desh.
  2. Ouma Fred Ogutu: Thunderstorm frequency over the Western Rift - Valley and Lake Victoria region of Kenya and its relation to aviation industry 10/1278/2012, tovuti ya University of Nairobi, Department of Meteorology, 2016
  3. "What places in the world have the most hail in one year". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2017-10-17. Iliwekwa mnamo 2018-02-20. {{cite web}}: Unknown parameter |= ignored (help)

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search