Mvua ya mawe (kwa Kiingereza hail) ni aina ya mvua ambayo matone ya maji yamefika kwenye uso wa ardhi kwa umbo la vipande vya barafu. Inatokea wakati matone ya maji ya mvua yanapita kwenye hewa baridi na kuganda hadi kuwa barafu.
Hali halisi mvua inayonyesha si mawe bali vipande vya barafu.
Tone zito zaidi lililowahi kupimwa lilinyesha sehemu za Gopalganj (Bangladesh) tarehe 14 Aprili 1986, likiwa la kilogramu 1.02[1]. Kericho nchini Kenya penye mvua ya radi mara nyingi[2] ni mahali ambako mvua ya mawe inanyesha zaidi kushinda sehemu nyingine za Dunia[3].
{{cite web}}
: Unknown parameter |=
ignored (help)
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search