Mwaka wa Kanisa

Mwaka wa Kanisa kadiri ya kalenda ya liturujia ya Roma kama kielelezo cha kawaida kwa Wakristo wa magharibi.
Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki


Mwaka wa Kanisa (pia: mwaka wa liturgia / liturujia) ni mpangilio wa maadhimisho au kalenda inayoratibu majira na sikukuu za Ukristo katika muda wa mwaka mmoja.

Kalenda hii inataja nafasi ya vipindi vya pekee kama vile Majilio (Adventi), Krismasi au Noeli, Kwaresima au Pasaka, pamoja na nafasi ya sikukuu mbalimbali.

Sikukuu kadhaa kama Krismasi zinafuata tarehe za kudumu za kalenda ya jua, lakini nyingine kama Pasaka tarehe zake zinazosogezwa katika kalenda ya kawaida, hasa kwa sababu zinafuata hesabu ya Jumapili, si tarehe katika mwezi fulani.

Mwendo wa vipindi vya liturujia unafanana na ule wa maisha ya binadamu, ambayo yana maadhimisho ya pekee na majira ya kukua na kukomaa kwa utulivu. Vivyo hivyo mwaka wa Kanisa una sikukuu na siku za kawaida, vipindi vya pekee na la.

Sehemu muhimu zaidi ya mwaka huo inategemea Pasaka na Krismasi, sherehe kuu mbili zinazoendesha muda mtakatifu wote, ingawa zimo sikukuu nyingine pia.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search