Mwalimu

Darasa la shule ya sekondari nchini Sierra Leone.
Mwalimu wa Kilatini na wanafunzi wake wawili, 1487

Mwalimu (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza teacher, school teacher na pengine educator) ni mtu anayesaidia wengine kupata ujuzi, maarifa na tunu.

Kazi hiyo inaweza kufanywa na yeyote katika nafasi maalumu, kwa mfano mzazi au ndugu akimfundisha mtoto nyumbani, lakini kwa wengine ndiyo njia ya kupata riziki inayomdai karibu kila siku kwa miaka mingi, kwa mfano shuleni. Huko mwalimu anatakiwa kuwa na shahada au stashahada, kadiri ya sheria za nchi na ya ngazi ya elimu inayotolewa.

Imesemekana kuwa walimu vijana wanafundisha kuliko wanavyojua, yaani hata mengi wasiyoyajua vizuri. Wenye umri wa makamo wanafundisha yale yote wanayoyajua. Kumbe wazee wanafundisha yale yanayowafaa wasikilizaji.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search