Nyasi

Nyasi
Nyasi
Nyasi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Monocots (Mimea ambayo mche wao una jani moja)
(bila tabaka): Commelinids (Mimea kama jaja)
Oda: Poales (Mimea kama nyasi)
Familia: Poaceae (Nyasi)
Ngazi za chini

Nusufamilia 12

Nyasi ni kundi la mimea inayofunika udongo; nyasi zilizo nyingi si kubwa sana lakini aina kama mianzi hufikia urefu wa miti. Kibiolojia hujumlishwa katika familia ya Poaceae au Gramineae.

Nyasi nyingi huwa na mizizi mirefu inayoshika ganda la juu la ardhi hivyo kuzuia au kupunguza mmomonyoko wa udongo. Kiekolojia aina za nyasi zimezoea mazingira tofauti kabisa kati ya kanda za joto hadi kanda za baridi sana. Wakati wa baridi au ukame majani juu ya ardhi hukauka hata kupotea kabisa lakini mizizi ina uwezo wa kulala muda mrefu na kusubiri mvua au halijoto ya juu zaidi.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search