Oksijeni


Oksijeni
Oksijeni ndani ya chupa katika hali ya kiowevu ikiwa na halijoto chini ya -182.95 °C
Oksijeni ndani ya chupa katika hali ya kiowevu ikiwa na halijoto chini ya -182.95 °C
Jina la Elementi Oksijeni
Alama O
Namba atomia 8
Mfululizo safu Simetali
Uzani atomia 15.9994
Ugumu (Mohs) {{{ugumu}}}
Kiwango cha kuyeyuka 54.36K (-218.79°C)
Kiwango cha kuchemka 90.20K (-182.95 °C)
Asilimia za ganda la dunia 49,4 %
Hali maada gesi

Oksijeni (en:oxygen) ni elementi simetali yenye namba atomia 8 na uzani atomia 15.9994 kwenye mfumo radidia. Alama yake ni O.

Ni kati ya elementi zilizopo kwa wingi ulimwenguni ikishika nafasi ya tatu baada ya hidrojeni na heli. Kwenye dunia yetu asilimia 28 za masi yake ni oksijeni; ni elementi iliyopo kwa wingi kabisa katika ganda la dunia.

Hutokea ama kama mchanganyiko wa elementi nyingine au pekee yake kama gesi isiyo na rangi wala herufi. Pekee yake hupatikana hasa kama molekuli ya O2 yaani mchanganyiko wa kikemia wa atomi mbili. Kuna pia oksijeni ambayo ni molekuli ya atomi tatu unaoitwa ozoni (O3).

Umuhimu wake duniani ni hasa kuwepo katika maji na katika hewa ya angahewa na kwa ujumla kwa ajili ya uhai. Karibu viumbe vyote duniani hutegemea oksijeni. Wanaipata ama kwa kupumua hewani au kwa kuichukua kwenye maji. Oksijeni tupu ni sumu kwa ajili ya viumbe vingi.

Kama atomi ya pekee ya oksijeni inakutana na atomi mbili za hidrojeni zinakuwa H2O (maji).


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search