Papa Pius V, O.P. (17 Januari 1504 – 1 Mei 1572) alikuwa Papa kuanzia tarehe 7/17 Januari 1566 hadi kifo chake[1]. Alitokea Alessandria, Italia[2].
Alimfuata Papa Pius IV akafuatwa na Papa Gregori XIII.
Umuhimu wake katika historia ya Kanisa ni kwamba ndiye alishughulikia kwa moyo wa ibada na bidii ya kitume utekelezaji wa Mtaguso wa Trento kwa ajili ya urekebisho wa Kikatoliki, ukiwa pamoja na vitabu vya liturujia, katekesi na maadili, ili kueneza imani.
Anaheshimiwa kama mtakatifu.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search