Pasaka

Meza ya Seder yaani Chakula cha Pasaka ya Kiyahudi ikionyesha vitabu vya Haggada.
Yesu mfufuka.
Mayai ya Pasaka.

Pasaka ni sikukuu muhimu katika dini za Uyahudi na Ukristo. Jina la Pasaka limetokana na neno la Kiebrania "פסח" (tamka: pasakh).

Taarifa za Agano Jipya zinatoa habari ya kuwa kufa na kufufuka kwa Yesu yametokea wakati wa sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi. Kwa hiyo jina la sikukuu hiyo limeendelea kutumika kwa ajili ya sherehe ya Kikristo.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search