Pomboo

Kwa kundinyota linalojulikana pia kama "delphinus" angalia Dalufnin (kundinyota)

Pomboo
Pomboo
Pomboo
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Cetacea (Wanyama kama nyangumi)
Oda ya chini: Odondoceti (Nyangumi wenye meno)
Ngazi za chini

Familia 7:

Pomboo (kwa Kiingereza dolphin) ni wanyama wa bahari wa familia mbalimbali katika oda ya Cetacea au nyangumi. Wanahesabiwa kati ya nyangumi wenye meno (Odondoceti).

Spishi nyingi zinaishi baharini lakini kuna pia spishi chache wanaokaa kwenye maji baridi ya mito. Kuna pia spishi za pomboo wa mtoni ambao ni familia tofauti hata wakifanana sana na pomboo za kawaida.

Kama nyangumi wote wana maisha yanayofanana na samaki lakini si samaki, bali mamalia wanaozaa watoto hai na kuwanyonyesha maziwa kwa kutumia viwele vyao. Wana damu moto na kupumua kwa mapafu, maana yake hawawezi kukaa chini ya maji muda wote kama samaki, bali wanapaswa kufika kwenye uso wa maji na kupumua kabla ya kuzama chini tena kwa muda mrefu.

Pomboo wanahesabiwa kati ya wanyama wengi akili sana, ijapokuwa ni vigumu kusema wanayo kiasi gani. Kujua kiwango cha akili kwa wanyama wengine, pomboo wamekwishafanyiwa tafiti nyingi wakiwa wanafugwa, au wanaishi peke yao. Aina kadhaa wana ubongo mkubwa sawa na mwanadamu, na ni marafiki wake wazuri, jambo linalowajengea umaarufu mkubwa.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search