Rasi ya Uarabuni

Bara Arabu kutoka angani.

Rasi ya Uarabuni (au:Bara Arabu) ni rasi kubwa iliyoko Asia ya Magharibi kati ya Bara la Afrika na Bara la Asia ambapo sehemu yake kubwa imezungukwa na bahari, upande wa magharibi Bahari ya Shamu, upande wa kusini na Bahari ya Hindi na ule wa Mashariki Ghuba ya Uajemi. Sehemu za Kaskazini mwa Bara Arabu zimepakana na nchi za ufalme wa Jordani na jamhuri ya Iraq.

Kwa macho ya gandunia rasi hii ni karibu sawa na bamba la Uarabuni.

Kwa sababu ya ukame, hakuna mito ya kudumu katika bara hili, ijapokuwa kwenye sehemu mbalimbali kunapatikana chemchemi na vijito vya maji ambavyo huzidi wakati wa msimu wa mvua katika majira ya baridi. Sehemu kubwa ni jangwa tu.

Bara Arabu ina milima upande wa Magharibi na Kusini, lakini kila ukiteremkia Mashariki unakutana na ardhi tambarare mpaka kufikia kwenye Ghuba ya Uajemi.

Katika karne ya 20 nchi za Uarabuni zilipata nafasi ya kutajirika kwa sababu ya mafuta mengi ya petroli yaliyo chini ya ardhi yao.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search