Sayari

Sayari za mfumo wa jua letu; ukubwa unaonyesha uwiano halisi kati ya sayari lakini umbali kati ya sayari hauonyeshwi.

Sayari (kwa Kiingereza planet) ni kiolwa kikubwa cha angani kinachozunguka jua (au nyota nyingine) na kung'aa kutokana na nuru ya jua iliyoakisiwa, tofauti na nyota na jua zinazong'aa peke yake. Kwa macho inaonekana kama nyota, lakini baada ya kuitazama kwa muda wa mwaka inaonekana inabadilisha mahali pake angani, tofauti na nyota kwa jumla. Tofauti kubwa kati ya sayari na nyota ni kwamba, nyota ukiitazama inametameta ila sayari haiwezi.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search