Songo Mnara

9°04′13″S 39°34′58″E / 9.0704°S 39.58288°E / -9.0704; 39.58288

Kwenye maghofu ya Songo Mnara.

Songo Mnara (pia: Songa Mnara, Songa Manara) ni kisiwa katika funguvisiwa la Kilwa, upande wa kusini mwa Kilwa Kisiwani. Kiutawala ni sehemu ya kata ya Pande Mikoma kwenye Wilaya ya Kilwa, Tanzania.

Upande wa mashariki wa kisiwa kuna maghofu ya mji wa kale wa Songo Mnara. Maghofu hayo yamekubaliwa pamoja na yale ya Kilwa Kisiwani katika orodha ya urithi wa dunia wa UNESCO.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search