Spishi

Ngazi za uainishaji katika biolojia; ngazi ndogo za kati hazionyeshwi

Spishi (kutoka Kilatini "species", yaani: aina, maumbile) katika biolojia ni jina la kutaja kundi la wanyama au mimea wa aina moja. Spishi ni kitengo muhimu katika uainishaji wa kisayansi.

Kwa kuhesabiwa katika spishi ileile haitoshi kama viumbe vinafanana sana, ni lazima waweze kuzaliana na kuwa na watoto ambao wanaweza kuzaa tena.

Kwa mfano, farasi na punda ni spishi mbili tofauti zinazoweza kuzaliana lakini watoto wao, wanaoitwa baghala, hawazai tena. Mbwa wote ni spishi moja, hata kama wanaonekana na maumbile tofauti kutokana na historia ya ufugaji wa kuteua sifa kadhaa tu kwa kuzaana. Lakini hata mbwa mkubwa kabisa anaweza kuzaliana na mbwa mdogo na watoto wao wanazaa tena.

Spishi za karibu hupangwa pamoja katika jenasi.

Mfano: mbwa, mbweha, mbweha wa Ethiopia na koyote wa Marekani wote ni spishi mbalimbali za jenasi inayoitwa "Canis".


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search