Teolojia ya Kiroho


Teolojia ya maisha ya kiroho ni tawi la teolojia linalohusu utekelezaji wa teolojia ya dogma na ya teolojia ya maadili katika kuongoza watu kuelekea muungano na Mungu ulio wa dhati zaidi na zaidi, likifafanua muungano huo ni nini na njia za kuufikia ni zipi. Hivyo linafafanua taratibu za ustawi wa uzima wa Kiroho kwa misingi ya teolojia (kwanza Biblia, lakini pia Mapokeo na Ualimu wa Kanisa) likiilinganisha na mang'amuzi ya watakatifu.

Kitengo hicho cha teolojia ni muhimu hasa kwa Wakatoliki na Waorthodoksi, ambao kwao muungano na Mungu ndio lengo la ufunuo wake kwa binadamu.

Madhehebu mengine ya Kikristo yana mtazamo tofauti kuhusu kumfuata Yesu Kristo kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search