Tertuliani

Tertuliani

Quintus Septimius Florens Tertullianus (160 hivi – 225 hivi),[1] alikuwa padri na mwandishi maarufu wa Ukristo wa mwanzoni kutoka Karthago, mji wa mkoa wa Afrika katika Dola la Roma, leo nchini Tunisia.[2]

Ndiye Mkristo wa kwanza aliyeandika sana kwa Kilatini, akiathiri fasihi yote iliyofuata hasa kwa misamiati yake mipya, hasa kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu[3] akaitwa "mwanzilishi wa teolojia ya Magharibi."[4]

Katika maandishi yake anajitokeza kama mtetezi wa imani pamoja na kupinga uzushi, ingawa ukali wa itikadi yake hatimaye ulimfanya ajitenge na Kanisa Katoliki[5].

Habari chache tulizonazo kuhusu maisha yake yanapatikana hasa katika maandishi yake.

  1. T.D.Barnes, Tertullian: a literary and historical study, Oxford, 1971
  2. T. D. Barnes, Tertullian: a Historical and Literary Study (Oxford: Clarendon Press, 1985), 58.
  3. Ekonomou 2007
  4. Justo L. Gonzáles, The Story of Christianity, Volume 1: The Early Church to the Dawn of the Reformation (New York: HarperCollins Publishers, 2010), 91–93.
  5. https://dacb.org/stories/tunisia/tertullian/

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search