Ubuddha

Sanamu kubwa ya Buddha kwenye kisiwa cha Lantau, Hong Kong, China).
Asilimia ya Wabuddha nchi kwa nchi, kadiri ya Pew Research Center, 2010.

Ubuddha ni mfumo wa kidini uliotokana na mafundisho ya Siddharta Gautama aliyejulikana kama Buddha.

Kuna wafuasi wengi, hasa katika Asia ya Kusini, Kusini-Mashariki na Mashariki. Makadirio ya idadi yao ni kati ya milioni 488-535 (7-8% ya watu wote duniani). Hivyo ni dini kubwa ya nne baada ya Ukristo, Uislamu na Uhindu.

Mafundisho yao yalianzishwa na Siddhartha Gautama aliyezaliwa mnamo mwaka 563 KK kufuatana na mapokeo; wataalamu wengine huona ya kwamba alizaliwa karne moja baadaye.

Wanahistoria wengi wa mwanzo wa karne ya 20 walitaja miaka 563 KK hadi 483 KK hivi,[1] lakini maoni ya siku hizi yanataja mwaka wa kufariki kati ya 486 KK na 483 KK au, hata kati ya 411 KK na 400 KK.[2][3]

Kadiri ya akiolojia, Buddha aliweza kuzaliwa huko Lumbini, (leo nchini Nepal)[4][5][4] au huko Kapilavastu, Piprahwa, Uttar Pradesh, India au tena Kapileswara, Orissa, India.[6][7][8][9][10]

Anaitwa pia "Buddha wa kihistoria" au "Buddha Shakyamuni" kwa sababu katika imani yao kuna mabuddha mbalimbali.

Neno "Buddha" si jina bali cheo cha heshima chenye maana ya "aliyeamka". Humo mna kiini cha imani ya Ubuddha kuwa binadamu huishi kwa kawaida bila ya kutambua hali yake mwenyewe, lakini akielewa mafundisho anakuja kuamka na kuona hali yake pamoja na njia inayopaswa kufuatwa.

Katika haya yote Wabuddha hufuata mfano wa Buddha Shakyamuni wakitegemea kufika kwenye hali ya kuamka.

Kati ya Wabuddha kuna mielekeo mbalimbali kama madhehebu. Yale yenye wafuasi wengi ni:

  1. L. S. Cousins (1996), "The dating of the historical Buddha Archived 26 Februari 2011 at the Wayback Machine.: a review article", Journal of the Royal Asiatic Society (3)6(1): 57–63.
  2. See the consensus in the essays by leading scholars in The Date of the Historical Śākyamuni Buddha (2003) Edited by A. K. Narain. B. R. Publishing Corporation, New Delhi. ISBN 81-7646-353-1.
  3. "If, as is now almost universally accepted by informed Indological scholarship, a re-examination of early Buddhist historical material, ..., necessitates a redating of the Buddha's death to between 411 and 400 BCE...." —Paul Dundas, The Jains, 2nd edition, (Routledge, 2001), p. 24.
  4. 4.0 4.1 "Lumbini, the Birthplace of the Lord Buddha". UNESCO. Iliwekwa mnamo 26 Mei 2011.
  5. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2012-10-31. Iliwekwa mnamo 2015-01-21.
  6. "Kapilavastu". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-01-08. Iliwekwa mnamo 1 Machi 2011.
  7. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2013-06-03. Iliwekwa mnamo 2015-01-21.
  8. http://www.rediff.com/news/2002/sep/16spec.htm
  9. http://www.srilankaguardian.org/2008/03/buddha-born-in-orissa-scholars.html
  10. "Nakala iliyohifadhiwa" (PDF). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 2012-03-18. Iliwekwa mnamo 2015-01-21.

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search