Uhindi

भारत गणराज्य
Bhārata Gaṇarājya

Jamhuri ya Uhindi
Bendera ya Uhindi Nembo ya Uhindi
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: "Satyameva Jayate" (Kisanskrit)
Kidevanāgarī: सत्यमेव जयते
("Ukweli pekee hushinda")
Wimbo wa taifa: "Jana Gana Mana"
Lokeshen ya Uhindi
Mji mkuu New Delhi
28°34′ N 77°12′ E
Mji mkubwa nchini Mumbai
Lugha rasmi Kihindi, Kiingereza na lugha nyingine 21
Serikali Jamhuri ya Maungano
Ram Nath Kovind
Narendra Modi
Uhuru
-ndani ya Jumuiya ya madola
-kama Jamhuri
Kutoka Uingereza
15 Agosti 1947
26 Januari 1950
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
3,287,590 km² (ya 7)
9.6
Idadi ya watu
 - 2018 kadirio
 - 2011 sensa
 - Msongamano wa watu
 
1,352,642,280 (ya 2)
1,210,193,422
384.8/km² (ya 31)
Fedha Rupia (Rs.)1 (INR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
IST (UTC+5:30)
not observed (UTC+5:30)
Intaneti TLD .in
Kodi ya simu +91

-

1 Re. is singular


India katika mipaka yake iliyokubaliwa na wote, bila maeneo yanayogombaniwa na nchi tofauti.

Uhindi (pia: India) ni nchi kubwa ya bara la Asia, upande wa kusini, ikienea hasa katika rasi kubwa ya Bahari ya Hindi.

Kwa eneo ina nafasi ya saba duniani, lakini kwa idadi ya wakazi (1,352,642,280 mwaka 2018) ni nchi ya pili baada ya China. Kati ya nchi za kidemokrasia ndiyo yenye watu wengi zaidi duniani. Tena inakadiriwa kwamba miaka ya hivi karibuni itapiku China.

Imepakana na Pakistan, China, Nepal, Bhutan, Bangladesh na Myanmar.

Kiutawala Uhindi ni shirikisho la jamhuri lenye majimbo ya kujitawala 29 pamoja na maeneo ya shirikisho 7.

Mji mkuu ni New Delhi, lakini mji mkubwa zaidi ni Mumbai.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search