Uhuru Kenyatta

Picha yake.

Uhuru Muigai Kenyatta (amezaliwa 26 Oktoba 1961) ni mwanasiasa nchini Kenya ambaye amekuwa rais wa nne wa Jamhuri ya Kenya kuanzia tarehe 9 Aprili 2013 mpaka tarehe 13 Septemba 2022.

Uhuru alihudumu kama mbunge wa Gatundu Kusini kuanzia mwaka wa 2002 hadi 2013. Pia alihudumu kama naibu waziri mkuu kuanzia 2007 hadi 2013.

Uhuru alihusika na chama cha Kenya Africa National Union (KANU) hapo awali kabla ya kubuni chama cha The National Alliance (TNA). Chama hicho kiliungana na kile cha United Republican Party (URP) kikiongozwa na William Samoei Ruto ili kubuni chama cha Jubilee, kilichompa Uhuru kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa 2013, naye William Ruto akichaguliwa kama naibu rais.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search