Uislamu

Uislamu
الإسلام (Al-Islām)

ukubwa_wa_picha
Hilali na Nyota, ishara ya Uislamu

Uainishaji ya Ibrahimu
Maandiko Qur'an
Hadith
Teolojia Mungu mmoja (Allah)
Eneo Duniani kote, hasa Mashariki ya Kati, Asia ya Kusini, Afrika Kaskazini
Lugha Kiarabu cha Qur'an
Mwaasisi Mtume Muhammad
Asili Karne ya 7 BK, Arabia
Ibada Sala, Saumu, Zaka, Hija, Shahada
Wafuasi Bilioni 1.9[1]
Kaaba ni kibla ya Waislamu wote duniani wakati wa swala.

Uislamu (kwa Kiarabu: الإسلام Al-Islām) ni dini inayotokana na mafunzo ya Mtume Muhammad. Wafuasi wa imani hiyo huitwa "Waislamu" na wanakadiriwa kuwa milioni 1,800 hivi. Hivyo ni dini ya pili duniani yenye wafuasi wengi baada ya Ukristo wenye wafuasi milioni 2,400.

Uislamu ni ile imani kuwa muumba ni mmoja tu kwa dhati na sifa zake. Nguzo nyingine za imani zinajengwa juu ya imani ya Mungu mmoja wa kweli, imani juu ya maisha baada ya kifo, imani juu ya Malaika wa Mungu, vitabu vyake na kudra na tafsiri ya vitendo ya imani hii ni: Sala, Zakah, Saumu na Hija.

  1. Pew Research. "Watu kulingana na Dini" (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-02-18.

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search