Ukomunisti

Nyundo na Mundu, ni alama ya ukomunisti, nguvu ya wafanyakazi.

Ukomunisti ni njia ya kisiasa ya kufikiri na dhana ya jinsi gani jamii inapaswa kufanya kazi na kupanga mambo yake.

Ukomunisti ni aina ya ushoshalisti ambao unasema haipaswi kuwa na tofauti za matabaka katika jamii.

Ukomunisti unasema watu wa kila sehemu ya dunia wanapaswa kumiliki zana, viwanda, na mashamba ambayo yanatumiwa kuzalishia bidhaa na vyakula. Mchakato huu wa kijamii hujulikana kama umiliki wa kawaida. Katika jumuia ya wakomunisti, hakuna mali binafsi.

Mwanzo wa mafundisho haya uko kwenye maandiko ya Karl Marx na Friedrich Engels tangu kutolewa kwa "Ilani ya Kikomunisti" mwaka 1847[1].

  1. Maelezo ya Chama cha Kikomunist,

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search