Umeme

Radi angani inafuatana na mwanga wa umeme unaoonekana kwa macho.
Usambazaji wa umeme kwa njia ya nguzo

Umeme au stima hutokea wakati chaji ya umeme inatiririka. Ni chanzo cha nishati tunayotumia kwa kuendesha mashine na vifaa vingi.

Kiasili neno la Kiswahili "umeme" lilimaanisha mwangaza wa ghafla unaofuatana na radi angani, lakini katika Kiswahili cha kisasa hutumiwa zaidi kwa habari ya kisayansi na ya kitekinolojia inayoelezwa hapa.

Kwa maana ya kisayansi umeme ni neno pana sana linalojumlisha mambo mbalimbali ambayo yote yanahusiana na kuwepo kwa chaji ya umeme.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search