Unyenyekevu

Ishara ya Unyenyekevu katika kioo cha rangi, kazi ya Edward Burne-Jones.

Unyenyekevu (kutoka kitenzi "kunyenyekea"; neno la Kiingereza "humility" linatokana na Kilatini humilitas, ambapo mzizi ni humus, udongo. Sababu ni kwamba unyenyekevu ni kuelekea chini.[1]) ni hali ya kujishusha mbele ya wengine, hasa wakubwa au wanaostahili heshima ya pekee, kama vile Mungu.

Lengo la kufanya hivyo ni kukubali ukweli, kinyume cha kinavyotaka kiburi, kinavyojitahidi kujikuza bila haki.

Kati ya kweli zinazomhusu binadamu kuna udogo wake kimaumbile na ukosefu wake kimaadili. Ndizo zinazomdai anyenyekee kama adili la msingi.

  1. "Humble" from Merriam-Webster, m-w.com

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search