Utumwa

Picha ya mvulana mtumwa huko Zanzibar, 1890 hivi.

Utumwa ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kummiliki binadamu mwenzake kama mali yake. Binadamu anayemilikiwa anakuwa na hadhi sawa na chombo au kifaa chochote kinachoweza kuuzwa.

Mfumo huu ulianza kabla ya uandishi kubuniwa, ukawa maarufu hasa kabla ya harakati za ukoloni duniani, mathalani kuanzia karne ya 15, ambapo watumwa walihitajika katika shughuli za kilimo na uchimbaji madini katika sehemu mbalimbali za ulimwengu, hasa Amerika, ingawa katika sehemu nyingine, hasa Uarabuni, walitafutwa hasa watumwa wanawake kwa ajili ya uasherati.

Mfumo huu huunda matabaka ya "mabwana" ambao humiliki watumwa na "watwana" ambao ni watumwa wenyewe.


© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search