Wakabwa (au Wakabhwa, matamshi ambayo ni sahihi zaidi) ni kabila la watu wa Tanzania linaloishi katika Mkoa wa Mara. Lugha yao ni Kikabwa.
Idadi yao ni takribani watu 6000.
Wanapatikana katika vijiji vya Bukabwa, Mmazami (hapa wamechanganyika na Wazanaki, au 'Abhazanake', au 'Abhashanake'), Kamugendi (hapa wamechanganyika na Wazanaki na Wairege), na Kirumi (hapa wamechanganyika na Wakiroba au 'Abhakerobha').
Kama ilivyo kwa wakazi wengi wa Mkoa wa Mara, Wakabwa ni jamii au ukoo wa kabila kubwa la Wakurya. Mila na desturi zao zinaelekeana na koo nyingine za Kikurya. Lugha yao haina tofauti na makabila yanayojiita makabila ya Kikurya ijapokuwa ni koo tu. Matamshi yao yanaelekeana na Wasweta ambao hupatikana kwa wingi wilaya ya Tarime kando ya ziwa Victoria, jirani na Wasimbiti (Abhasimbete).
Kuna koo kubwa za Warimba, Washora na Waruhu.
Shughuli zao kubwa ni ukulima wa uwele, mtama, mhogo na ufugaji wa wanyama mbalimbali kama ng'ombe, mbuzi na kondoo.
Ni watu wanaomini sana kuhusu uchawi, ndiyo maana hata vijiji vyao vimeshindwa kufanya maendeleo ya haraka kwa kuhofia kulogwa.
Wengi wao wanapatikana katika kijiji cha magana na kirumi. Wanatahiri wanaume na kukeketa wasichana, ingawa mila hii ya kukeketa wasichana inaelekea kwisha.
Kuna milima kama Kimange, Magana, Misisya na Kweswa na kuna mito kama Nyamirama.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search