Yudea (kwa Kilatini IVDAEA, kwa Kiebrania יהודה, Yehûḏāh au Yehuda, kwa Kigiriki Ἰουδαία) ni jina la jimbo la Dola la Roma kuanzia mwaka 6 hadi 135 BK.
Iliunganisha Uyahudi wenyewe, Samaria na Idumea chini ya liwali.
Asili ya jina ni kabila la Yuda, ambalo kuanzia karne ya 8 KK lilibaki karibu peke yake kati ya makabila 12 ya Israeli.
© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search